Posts

Showing posts from December, 2011

MZEE MWENYE HEKIMA NA BUSARA

Hapo zamani kulikuwa na Mzee mmoja mwenye busara sana, alikuwa akiishi kwenye kijiji kimoja huko nchini Korea. Aliishi maisha ya tabu sana, ambapo aliweza kujifunza sana kutokana na maisha hayo, alikuwa akitumia akili nyingi na kufikiri kwa kina sana kutatua changamoto zilizokua zikimkuta. Watu kutoka sehemu mbalimbali walimfuata na kumuomba ushauri juu ya matatizo yao. Alikuwa akisikiliza kwa umakini na unyenyekevu mkubwa sana na hata alipokuwa akitoa ushauri alikua akitoa kwa umakini na hekima pia. Hii ilifanya watu wengi zaidi kumfuata kutoka sehemu za mbali sana kuja kuwa karibu na kuzungumza nae. Kulikuwa na Kijana mmoja pale kijijini, aliwashangaa watu wanaosafiri kwenda kuzungumza na huyo Mzee, “Anaujuzi ganu huyo mzee?” alikua akisema huyo kijana. “Hakusoma hata dirasa moja, na siamini kama anahekima kiasi gani watu wamfuate!” pindi akijiuliza kichwani kwake akapata wazo la kwenda kujaribu hiyo hekima ya yule mzee. Yule Kijana alikwenda porini na kukamata ndege mdogo, alafu...

JE UNAIJUA NYUMBA YAKO YA BAADAE?

Mzee mmoja engineer alikua amekalibia umri wake wa kustaafu, baada ya kufanya kazi ya ujenzi kwa muda mrefu sana. Alikua anamalengo ya kushi maisha ya nafasi na furaha yeye na familia yake baada ya kustafu. Alikua tayari kutopokea malipo yake ya cheki baada ya kila wiki aliyozoea, kwaajili tu ya Kustaafu. Yule Mzee akaamua kuandika ombi la kustaafu kwa Bosi wake. Mwajiri wake alisononeka sana kupata taarifa hizo, mfanyakazi wake mzuri anataka kustaafu. Yule Mwajiri alikwenda kumuomba Yule Mzee kama angeliweza kujenga nyumba moja ya mwisho kama personal favor. Yule engineer alikubali kufanya kazi hiyo ya mwisho, lakini ilionekana wazi kabisa kuwa moyo wake haukuridhia kazi hiyo, alifanya kazi kwa ubunifu na ubora wa chini na kutumia material dhaifu kabisa. Yaani ilikuwa wazi kabisa kuwa hana haja tena na kazi yoyote ya namna hiyo. Alipomaliza kujenga, mwajiri wake alikwenda kuikagua ile nyumba. Alafu akamkabidhi funguo funguo za nyumba hiyo yule Mzee na akamwambia,”Hii ni nyumba ...

MAMA NA MBWA

Katika kijiji fulani Kulikua na mama mmoja alikua akiishi na Mtoto na Mbwa mmoja mweupe mzuri sana. Yule mama alikua akitoka pale kijijini kwenda safari ndefu kutafuta riziki yake na mtoto wake mdogo. Pindi alipokua akitoka nyumbani alikua akimuacha mtoto wake na mbwa akimlinda mtoto huyo na mzingira ya kila kitu ya pale nyumbani hadi anapoludi. Siku moja yule mama alimuacha mtoto wake nje na kwenda sokoni mara moja. Alipoludi alimkuta mbwa wake ameloa damu na zingine zikivuja kwenye kucha na mdomoni.Yule mama alikimbia kumuangalia kama mtoto wake yupo salama pale alipomueka, akakuta kulikua na purukushani na damu zimedondoka na mtoto wake hayupo. Alilia sana yule mama na akachukua fimbo moja kubwa sana kwenda kumpiga yule Mbwa hadi kufa. Wakati akiludi ndani baada ya hilo tukio alimkuta mtoto wake chini ya kitanda akiwa salama kabisa na pembeni yake kulikua na mnyama mkali amekufa akiwa na majeraha. Hii ni hadithi fupi, lakini inaujumbe mzito sana katika maisha ya kila siku. Wang...