Posts

Showing posts from April, 2018

NDOTO ZA MKOSAJI

Msichana mmoja alikuwa anaelekea sokoni huku akiwa amebeba ndoo ya maziwa kichwani kwake. Akiwa   anatembea   alipanga mengi kichwani kwake “Nikiuza haya maziwa nitapata pesa nyingi za kununua kuku mweupe,”   atanitagia mayai mengi, yatatotoa vifaranga vingi. Nitavikuza vizuri hadi vitage mayai mengi zaidi. Mayai yatakuwa mengi Zaidi na nitakuwa na kuku wengi watakao taga tena mayai na kutototoa   vifaranga vingi Zaidi.. Kwa muda mfupi tu nitakuwa tajiri, nitanunua vitu vya gharama. Nitavaa nguo za ghrarama kubwa na madini kuanzia shingoni hadi miguuni mwangu.   Na ikitokea siku moja niitaenda kwa Malkia, nitampelekea zawadi   adimu ya thamani sana kutoka Marekani.   Nitaingia kwenye Jumba lake la kifahari,   mikono yangu imejaa vito vya gharama, kwa heshima nitainamisha kichwa na kumsalimu Malkia na kumwambia,…" Kabla hajasema alichotaka kumwambia Malkia, akjikuta Amedondosha ndoo aliyobeba kichwani na kumwaga   maziwa yote yal...

MBWA MWITU NA MBUZI

Image
Kulikuwa na Mbuzi  Mmoja na Watoto wake saba. Siku moja alienda Msituni kutafuta chakula na kuwaacha watoto wake nyumbani. Lakini Kabla ya kuondoka, akawaonya watoto wake kuhusu “Mbweha” kwamba, kuna Mbweha Mkubwa Hatari sana, atakuja na kujaribu kuingia ndani ya nyumba na Kuwatafuna. Mbwa mwitu atajifanya kuwa mama yenu na kuwashawishi kufungua mlango. Watoto wa Mbuzi wataweza kumtambua mama yao wa kweli kwa miguu yake meupe na sauti nzuri na nyororo.  Yule Mama mbuzi akaondoka na kuwaacha watoto wake saba wakiwa ndani ya nyumba. Baada ya muda mfupi, wakasikia “ngo ngo ngo ngo” na sauti mlangoni   ambayo inasema "Nifungulieni mlango watoto wangu, nina zawadi kwa kila mmoja wenu". Sauti yake ilikuwa mbaya sana na watoto wakaogopa kufungua mlango. Mbwa mwitu akaenda kwenye soko na kuiba asali ili kuifanya sauti yake iwe nyororo. Muda mfupi baadaye, watoto wakasikia sauti nyingine mlangoni: "Nifungulieni mlango watoto wangu, mama yenu nina zawadi kwa kila ...