NDOTO ZA MKOSAJI


Msichana mmoja alikuwa anaelekea sokoni huku akiwa amebeba ndoo ya maziwa kichwani kwake.

Akiwa  anatembea  alipanga mengi kichwani kwake “Nikiuza haya maziwa nitapata pesa nyingi za kununua kuku mweupe,”  atanitagia mayai mengi, yatatotoa vifaranga vingi. Nitavikuza vizuri hadi vitage mayai mengi zaidi. Mayai yatakuwa mengi Zaidi na nitakuwa na kuku wengi watakao taga tena mayai na kutototoa  vifaranga vingi Zaidi..

Kwa muda mfupi tu nitakuwa tajiri, nitanunua vitu vya gharama. Nitavaa nguo za ghrarama kubwa na madini kuanzia shingoni hadi miguuni mwangu.  Na ikitokea siku moja niitaenda kwa Malkia, nitampelekea zawadi  adimu ya thamani sana kutoka Marekani.  Nitaingia kwenye Jumba lake la kifahari,  mikono yangu imejaa vito vya gharama, kwa heshima nitainamisha kichwa na kumsalimu Malkia na kumwambia,…"

Kabla hajasema alichotaka kumwambia Malkia, akjikuta Amedondosha ndoo aliyobeba kichwani na kumwaga  maziwa yote yaliyomo.

Comments

Popular posts from this blog

NANI ATAMFUNGA PAKA KENGERE?

WANYAMA NA TABIA ZA BINADAMU