MUONGO HAAMINIKI HATA AKISEMA UKWELI


Kulikuwa na kijana mmoja akichunga Kondoo wa kijiji juu ya kilima. Yule Kijana akajilaza juu ya kilima hiko akiwa amechoka na kuboreka  baada ya kuchunga wale kondoo kwa muda mrefu siku hiyo. Hivyo akafikiria kufanya kitu kitakacho mchangamsha.  
Akavuta pumzi  kuubwa na kupiga kelele, “Simba! Simba! Simba!  Huku akiwafukuza wale kondoo.
Wanakijiji walikuja wakikimbia juu ya kilima ili kumsaidia yule kijana. Lakini walipofika juu, hawakukuta simba.  Yule kijana aliwacheka mbele ya nyuso zao zilizo jaa hasira.
Wale wanakijiji wakamwambia yule kujana "Usipige kelele za Simba wakati hakuna Simba !", Wakashuka chini ya mlima huku wamekasirika.
Baadaye, kijana huyo alipiga kelele za simba tena, "Simba! Simba anakimbiza kondoo!” Kwa furaha yake mbaya, aliwaangalia wanakijiji wakipanda tena kile kilima ili kumsaidia kufukuza Simba.
Wanakijiji walipofika juu pasi na kuona Simba, wakasema kwa ukali, "Piga kelele za kuomba msaada wakati kuna kitu cha Hatari kweli! Usipige kelele za ‘Simba’ wakati hakuna Simba!"
Lakini Yule mvulana alidharau na kucheka wakati wanakijiji wakishuka chini ya kilima kwa hasira.
Baadaye, aliona Simba wa kweli akinyemelea Kundi la kondoo kule kilimani. Yule kijana alichanganyikiwa na kuanza kupiga kelele kwa nguvu na sauti kubwa kuliko awali, “Simba! Simba! Simba!”
Lakini wanakijiji walidhani alikuwa anajaribu kuwadanganya tena, na hivyo hawakuenda kutoa msaada.
Jua lilipozama, kila mtu alijiuliza kwa nini mvulana huyo mchungaji hakurudi kijiji na kondoo wao. Walipanda kilima ili kumtafuta. Hatimae wakamkuta akilia.
"Simba alikuja hapa kweli! Kondoo wote wametawanyika!" Nililia, "Simba!" Kwa nini humkuja kunisaidia? "
Mzee mmoja alijaribu kumfariji yule kijana wakati  wanaludi kijijini.
"Tutakusaidia kutafuta kondoo waliopotea kesho asubuhi," alimwambia, uku akizungusha mkono wake juu ya bega la yule kijana, "Hakuna mtu anayemuamini mwongo .. hata pale anaposema ukweli!"

Comments

Popular posts from this blog

NANI ATAMFUNGA PAKA KENGERE?

WANYAMA NA TABIA ZA BINADAMU