HAKUNA KAMA MAMA


Baada ya kumaliza Masomo yake, aliamua kuaga wazazi wake na kwenda Mjini kutafuta maisha.
Alipofika mjini aliajiriwa kwenye kampuni ya Wachina, malipo ya mshahara wake yalikuwa madogo sana hayakuweza kukidhi mahitaji yake ya mwezi, ilikuwa ikifika katikati ya mwezi hata nauli ya kwenda kazini ilikuwa inakosekana. Lakini alijitahidi kujinyima, kidogo alichokipata alikuwa akihifadhi na kila alipokuwa akiwatembelea wazazi wake alikuwa anawapelekea pesa kidogo na kuludi mjini kuendelea na maisha yake.
Yule kijana alijiwekea malengo baada ya miaka mitatu aweze kuwa na mtaji wa kufanya biashara itakayo ongeza kipato  mbali na kile cha kuajiriwa.  Kila alipokuwa akimpigia simu Mama yake, cha kwanza alikuwa akiulizwa maendeleo ya mipango hiyo.  Majibu hayakuwa mazuri. Hakuna alichokuwa anakibakisha kila mwezi, ilikuwa ni ngumu kutokana maisha ya mjini, ila pamoja na hayo yote alikuwa lazima akawaone wazazi wake na kumwachia mama yake kiasi cha pesa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.
Baada ya Miaka Mitatu, yule kijana  hakuweza kutimiza malengo yake. Alienda kuwatembelea wazazi wake kama kawaida yake. Katikati ya Maongezi yao, Mama yake akamuuliza maendeleo yake pamoja na Mipango ya biashara aliyotaka kuifanya. Majibu yake yalikuwa yakukata tamaa na alipanga kutafuta kazi nyingine yenye kipato kikubwa zaidi ya anachopata kwa sasa.
Mama yake, akamwambia subili niingie ndani kuna ujumbe wako nikupe. Mama akaingia ndani na kutoka na Kiasi cha Pesa alichokuwa akihitaji kwa ajili ya biashara yake. 
Yule kijana alipigwa butwaa, akamuuliza mama yake, “mama umepata wapi pesa zote hizi? na hali ya maisha yako binafsi sio nzuri, hadi mimi nikuletee pesa kutoka mjini.” 
Mama akamjibu, “ulipokuwa unaniambia hali ya maisha yako sio nzuri kutokana na kipato chako, pesa zote ulizokuwa unaniletea nilikuwa nakuhifadhia mwanangu, sikuwahi kutumia hata kidogo, najua una moyo wa kutusaidia na kututunza wazazi wako lakini mafanikio yako ni furaha kwetu wazazi wako"

Comments

Popular posts from this blog

NANI ATAMFUNGA PAKA KENGERE?

WANYAMA NA TABIA ZA BINADAMU