TENDA WEMA UENDE ZAKO

Daktari aliingia hospitalini kwa haraka sana baada ya kuitwa kwa shughuli ya Upasuaji wa haraka. Aliingia chumba cha kubadilisha Mavazi na kuvaa nguo za kazi na kuelekea  moja kwa moja kwenye chumba cha upasuaji.

Wakati akielekea kwenye chumba cha upasuaji alimkuta Baba Mmoja anazunguka huku na huku karibu na chumba cha upasuaji akimsubiria Daktari. Baada ya kumuona tu, Yule Baba akapayuka: “ Kwanini umechelewa kuja? Hufahamu kama maisha ya Mtoto wangu yapo hatarini? Hivi unayajua majukumu yako?”

Yule Daktari alitabasamu na kumwambia: “ Samahani sana, Sikuwa Karibu na Hospitali na nimejitahidi kuja kwa haraka sana baada ya kupokea simu kutoka hapa hospitalini….. Na kwakuwa nimeshafika ningekuomba upunguze Jaziba na hasira ili nifanye shughuli yangu”

“ Punguza hasira?! Hivi ingekuwaje Mwanao ndiye angekuwa chumba cha upasuaji sasa hivi, ungeweza kupunguza hasira? Kama mwanao ndie anakufa sasa hivi ungefanyaje?” Yule Baba aliongea kwa hasira sana.

Yule Daktari alitabasamu tena na kumjibu: “ ningesema kama vitabu vinavotuambia tuseme, “ tumeumbwa kwa vumbi na tutaondoka kwa Vumbi, Jina la Mwenyezi Mungu Litukuzwe”.  Dactari hawezi kurefusha maisha ya Binadamu. Nenda katulie na umuombee mwanao, sisi tutajitahidi kadri kwa uwezo tulionao kwa Baraka za M.Mungu”

“ Kutoa Ushauri kwa vitu visivyo wahusu ni rahisi sana”  Alinong’ona Yule Baba mwenye mtoto mgonjwa.

Upasuaji ulifanyika kwa Masaa kadhaa mara tu baada ya kumalizika Daktari alitoka akiwa anafuraha, “ Asante Mungu! Mtoto wako tumeweza kumponya!”  Kama una swali lolote utamuuliza Nesi!!” Bila ya kumsikia Baba Mwenye mtoto kujibu chochote aliondoka kwa haraka kwenye eneo la upasuaji.

“ Kwa nini ni Mkorofi sana huyu Daktari? Yaani Hawezi hata kusubiri kidogo nimuulize maendeleo ya Mwanangu”  alimjadili akiwa na nurse baada ya Daktari kuondoka.

Nesi akamjibu, huku akitokwa na machozi: “ Mtoto wake alifariki jana kwenye ajari ya gari, hivyo alikuwa katika mazishi ya Mtoto wake wakati tunampigia simu aje hospitali kwa ajili ya Upasuaji wa Mtoto wako.  Amefanikiwa kuyaokoa maisha ya Mtoto wako, kwahiyo ameondoka kuwahi mazishi ya mtoto wake.”

Toleo la kwanza limeandikwa na ALLEGREI A. FERNANDO

HEKIMA:
“USI MUHUKUMU MTU YEYOTE…. SABABU HUYAJUI MAISHA YAO NA KIPI KILICHO WAKUTA KWENYE MAISHA YAO.
“ TENDA WEMA KADRI UWEZAVYO BILA YA KUJALI HALI ULIYONAYO”


Comments

Popular posts from this blog

NANI ATAMFUNGA PAKA KENGERE?

WANYAMA NA TABIA ZA BINADAMU